2012-07-28 21:14:28 VIEWED 1502 TIMES

Young Africans imefanikiwa kunyakua Ubingwa wa Vilabu kwa nchi za Ukanda wa Afrika Mshariki mara baada ya kuifunga timu ya Azam FC kwa mabao 2 - 0, katika mchezo wa fainali uliochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Mchezo huo ulioanza majira ya saa 10 jioni kwa saa za Afrika Mashariki, ulitanguliwa na mchezo wa kusaka mshindi wa tatu ai ya timu ya APR kutoka Rwanda na As Vita kutoka nchini DRC, ambapo As Vita illifanikiwa kuifunga APR kwa mabao 2-1 na kuwa mshindi wa tatu katika mashindao hayo,
Azam Fc iliyouanz amchezo huo kwa kasi, ilifanya mashambulizi ya mara kwa mara langoni mwa Young Africans ikisaka bao la mapema, lakini umakini wa walinzi wa Young Africans ulikuwa kikwazo kwa washambuliaji John Boko na Kipre Tcheche.
Huku Azam ikiendelea kuutawala mchezo kwa dakika 30 za kipindi cha kwanza, dakika ya 32 nusura Haruna Niyonzima aipatie timu yake bao la kuongoza lakini shuti lake hafifu lilidakwa na mlinda mlango wa timu ya Azam fc Deogratius Munsihi 'Dida'.

Young Africans ilibadilika na kuendelea kufanya mashambulizi langoni mwa timu ya Azam na katika dakika ya 44, Hamis Kiiza 'Diego' aliipatia Young Africans bao la kwanza, baada ya kuunasa mpira uliopigwa na mlinzi Aggrey Morris aiyekuwa akimrudishia golikipa wake na Kiiza kuuwahi na kuuweka kimiana na kuandika bao la kwanza.
Mpaka mpira unakwenda mapumziko Young Africans ilikuwa mbele kwa bao 1 - 0.
Kipindi cha pili kilianza kwa Azam fc kufanya mabadiliko amabapo iliwatoa Jabir Aziz na Kipre Tcheche na nafasi zao kuchukuliwa na Haji Nuhu na Mrisho Ngasa ambao bado hawakuweza kuubadili mchezo.
Azam fc nusura ipate bao la kusawazisha kupitia kwa mmshambuliaji wake John Boko, lakini mpira wa kichwa aliopiga kuelekea langoni uliokolewa na mlinzi Stephano Mwasika amaby leo alicheza nafasi ya mlinzi wa kulia ili hali akitumia mguu wa kushoto.
Dakika ya 62, Haruna Niyonzima alikosa tena bao la wazi kufuatia kazi nzuri iiyofanywa na Said Bahanunzi ,lakini Niyonzima alipiga shuti kubwa akiwa yeye a mlinda mlango wa Azam na kupaisha juu ya lango na kuwa mpira wa kutoka.
Rashid Gumbo alioka dakika ya 73 na nafasi yake kuchukuliwa na Juma Seif Kijiko, ambapo Young Africans iliendelea kuutawala mchezo kipindi chote za pili mpaka kuelekewa dakika za lala salama.
Huku washabiki , wapenz na wanachama wa Young Africans wakiianza kutoka nje wakijua tayari mpira umekwisha, Said Bahanunzi aliipatia Young Africans bao la pili kwa shuti kali kufuatia kuwatoka walinzi wa Azam na kumtungua Dida kwa shuti kali la mguu wa kushoto na kutinga nyavu za juu.
Mpaka mchezo unamalizika Young Afrians 2- 0 Azam .
Young Africans imefanikiwa kutwa Ubingwa huu kwa mara ya pili mfululizobaada ya kulichukua mwaka jana katika mchezo uliofanyika pia jijini Dar es salam na uwafunga Simba kwa bao 1- 0, bao la mshambuliaji kutoka nchini Ghana Kenneth Asamoah na ikiwa ni mara yake ya tano (5) tangu kuanzishwa kwake,

Said Bahanunzi ameibuka kuwa mfungaji bora wa mshindao hayo, baada ya kufunga jumla ya mabao sita (6) akifuatiwa na Teddy wa As Vita mwenye mabao sita pia lakini moja likiwa ni la penati na Hamis Kiiza ameibuka wa tatu kwa kufunga mabao tano (5).
Young Africans: 1.Ally Mustafa 'Barthez', 2.Stephao Mwasika, 3.Oscar Joshua, 4.Kelvin Yondani, 5.Nadir Haroub 'Cannavaro' (c), 6.Athuman Idd 'Chuji', 7.Rashid Gumbo/Juma Seif 'Kijiko', 8.Haruna Niyonzima, 9.Said Bahanunzi, 10.Hamis Kiiza 'Diego, 11.David Luhende
Azam FC: 1.Deogratius Munishi 'Dida', 2.Ibrahim Shikanda, 3.Erasto Nyoni, 4.Said Morad, 5.Aggrey Morris, 6.Jabir Aziz/Haji Nuhu, 7.Ibrahim Mwaipopo, 8.Salum Abubakar, 9.John Boko, 10.Kipre Tcheche/Mrisho Ngassa, 11.Ramadhani Chombo 'Redondo.
















