You are here: Home NEWS Local News NUSU FAINALI KAGAME 2012, YANGA Vs APR, AZAM Vs AS VITA

NUSU FAINALI KAGAME 2012, YANGA Vs APR, AZAM Vs AS VITA

E-mail Print PDF

2012-07-25     15:07:18    VIEWED 744 TIMES

Mashindano ya Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati almaarufu Kombe la Kagame 2012, yamefikia hatua ya Nusu Fainali ambapo timu nne(4) zitachuana siku ya alhamis kusaka timu timu mbili ambazo zitacheza fainali siku ya jumamosi katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

 

 

Mabingwa watetezi wa kombe hilo klabu ya Young Africans itashuka dimbani kucheza na tim ya APR kutoka Rwanda katika nusu fainali ya pili itakayofanyika jioni majira ya saa 10:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Nusu Fainali ya kwanza itaanza majira ya saa 8:00 mchana kwa kuzikutanisha timu za Azam FC (Tanzania) na timu ya AS Vita ya (DRC), timu ya Azam imefanikiwa kuingia hatua ya nusu fainali baada ya kuitoa timu ya Simba SC ya Tanzania pia kwa jumla ya mabao 3-1.

AS Vita nayo imefanikiwa kufika hatua hiyo ya nusu fainali baada ya kuifunga timu ya Atletico FC ya nchini Burundi kwa mabao 2-1 katika mchezo uliochzwa hapo awali.

Young Africans iimefanikiwa kufika hatua ya nusu fainali baada ya kuitoa timu ya Mafunzo ya Zanzibar kwa mikwaju ya penati 5-3, kufuatia kumalizika kwa dakika 90, ztimu zote zikiwa sare ya mabao 1-1.

APR kutoka Rwanda iliifinga timu ya URA kutok Uganda mabao 2-0 katika mchezo wa robo fainali na hivyo kupata tiketi ya kucheza hatua ya nusu fainali.

Kocha mkuu wa Young Africans Tom Saintfiet akiongea na tovuti ya klabu wwww.youngafricans.co.tz alisema anajua mchezo dhidi ya APR ni mgumu, kwani mchezo wa kwanza tulishinda kwa mabao 2-0, hivyo naamini APR wataingia Uwanjani wakiwa na nia ya kusaka ushindi tu ili waweze kucheza hatua ya fainali.

Saintfiet pia alisema pamoja na kuwa na mchezo huo mgumu dhidi ya APR, anaamin vijana wake wako katika hali nzuri ya ushindi, na maandalizi yote ya mchezo yamekamilika, hivyo anaamini timu yake Young Africans itaibuka na ushindi katika mchezo huo.

Mungu Ibariki Young Africans, Mungu Ibariki Tanzania.

'YANGA DAIMA MBELE, NYUMA MWIKO' 

Last Updated ( Wednesday, 25 July 2012 15:45 )  

 

   
  • FACEBOOK PAGE

  • TWITTER FEEDS

yanga1935: Uongozi wa mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Vodacom klabu ya Young Africans leo umekata mzizi wa fitina kwa kiungo... http://t.co/oZUqXpuAyz
yanga1935: Droo ya makundi kwa ajli ya mashindano ya Vilabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati al-maarufu kama (KAGAME CUP)... http://t.co/r2esjJLwtJ
yanga1935: Katibu Mkuu wa klabu ya Young Africans Lawrence Lawrence Mwalusako leo amemtambulisha rasmi kwa waandishi wa... http://t.co/fkfqNHiwz1
yanga1935: Green and yellow colours were dominant from the early hours of Saturday and it went on to be the dominant colours... http://t.co/sshr7bjgeQ
yanga1935: I posted 5 photos on Facebook in the album "CHAMP24NS" http://t.co/jw1L47m1kO
yanga1935: Sherehe za kukabidhiwa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2012/2013 kwa Mabingwa wapya Young Africans... http://t.co/S8GiejZjr7
yanga1935: Mpira umemalizika, Young Africans 2 - 0 Simba SC Kavumbagu ddk 4 Kiiza dkk 63
yanga1935: Dakika ya 89, Mpira umesimama kidogo, baada ya Nassoro Chollo kumsukuma Kavumbagu na wakati mwamuzi anamuulia kadondoka chini mwenyewe.
yanga1935: Dakika ya 85, anaingia Juma Abdul kuchukua nafasi ya Mbuyu Twite
yanga1935: Dakika ya 75, Young Africans 2 - 0 Simba SC Anaingia Nizar Khalfani kuchukua nafasi ya Hamis Kiiza
yanga1935: Dakika ya 75, Young Africans 1 - 0 Simba SC Anaingia Nizar Khalfani kuchukua nafasi ya Hamis Kiiza
yanga1935: Dakika ya 63, Hamis Kiiza anaipatia Young Africans bao la pili Young Africans 2 - Simba SC
yanga1935: Dakika ya 60, Young Africans 1 - 0 Simba SC
yanga1935: Kipindi cha pili cha mchezo kimeanza, Young Africans 1 - 0 Simba SC
yanga1935: KUMRADHI: bao la Yanga limefungwa na Didier Kavumbagu na sio Hamis Kiiza kama nilivyoandika awali
yanga1935: Mpira ni mapumziko, Young Africans 1 - 0 Simba SC
yanga1935: Dakika ya 30, Young Africans 1 - 0 Simba SC
yanga1935: Dakika ya 28 Simba walipata penati, akapiga Mussa Mudde na kukosa
yanga1935: Dakika ya 15, Young Africans 1 - 0 Simba SC
yanga1935: Dakika ya 4, Hamis Kiiza anaipatia Young Africans bao la kwanza
yanga1935: Mpira ndo umeanza hapa Uwanja wa Taifa kati ya wenyeji Simba SC Vs Young Africans
yanga1935: Heres Young Africans line-up to face Simba SC today: 1.Ally Mustapha - 1 2.Mbuyu Twite - 6 3.David Luhende - 29... http://t.co/XRMv18Y3vR
yanga1935: Vodacom Premier Leagu 2012/2013 Simba SC Vs Young Africans Kick-off 16:00hrs Venue: National Stadium #Tukutane... http://t.co/gD7xNq3rFs
yanga1935: Kikosi cha Mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara timu ya Young Africans leo kimefanya mazoezi yake... http://t.co/V6JQZYaJud
mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday2232
mod_vvisit_counterYesterday2489
mod_vvisit_counterThis week20334
mod_vvisit_counterLast week19559
mod_vvisit_counterThis month62678
mod_vvisit_counterLast month60138
mod_vvisit_counterAll days551708

We have: 182 guests, 4 bots online
Your IP: 54.242.188.217
 , 
Today: May 24, 2013