You are here: Home NEWS Local News YANGA KUIVAA AZAM JUMAMOSI

YANGA KUIVAA AZAM JUMAMOSI

E-mail Print PDF
2012-03-07       11:07:28         VIEWED 453 TIMES 
Kikosi cha Mabingwa wa ligi kuu Tanzania Bara Young Africans Sports Club kimeendelea na mazoezi katika viwanja wa vya shule ya Sekondari Loyola na shule ya IST kujiandaa na mchezo wa ligi kuu ya Vodacom dhidi ya timu ya Azam FC siku uya jumamosi katika uwanja wa Taifa jijini  Dar es salaam.
 
Young Africans ambayo mwishoni mwa wiki ilicheza na Zamalek ya Misri katika mchezo wa marudiano ya Kombe la Klabu Bingwa Afrika na kufungwa bao 1 - 0, ilirejea jumatatu asubuhi ambapo wachezaji walipewa mapumziko mpka siku ya jumanne walipoanza mazoezi ya pamoja.
 
Baada ya kutolewa katika mashindano ya kimataifa na Zamalek kwa jumla ya mabao 2-1, Young Africans inaelekeza nguvu zake katika kutetea Ubingwa wa ligi kuu ya Vodacom jumamosi kwa kucheza na Azam FC inayoshika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kuu nchini.
 
Kocha Mkuu Kostadian Papic amesema wachezaji wake walicheza vizuri katika mchezo wao jijini Cairo licha ya kufungwa bao 1- 0 na wenyeji wao, pia aliongeza kutolewa kwa Chuji kwa kadi nyekundu kulichangia timu kukosa ushindi kutokana na kucheza pungufu kwa mda mrefu huku akilalamikia hali ya hewa ya baridi iliyowasumbua wachezaji wake.
 
Katika kuhakikisha inaibuka na ushindi katika mchezo wa jumamosi Young Africans inaingia kambini leo jioni kwa ajili ya maandalizi ya mchezo huo wa jumamosi dhidi ya wana lamba lamba. 
 
Wachezaji wanaofanya mazoezi  ni pamoja na:
 
Walinda Milango; Shaban Hassan Kado, Said Mohamed,
 
Walinzi wa Pemebeni; Shadrack Nsajigwa, Godfrey Taita, Oscar Joshua, Abuu Ubwa, Stephano Mwasika,
 
Walinzi wa Kati; Chacha Marwa, Ibrahim Job, Bakari Mbega, Nadir Haroub Cannavaro, Zuberi Ubwa,
 
Viungo wa Ulinzi; Juma Seif Kijiko, Godfrey Bonny,Athuman Iddy Chuji
 
Viungo Washambuliaji; Haruna Niyonzima, Nurdin Bakari, Rashid Gumbo, Athuman iddy Chuji
 
Viungo wa Pembeni; Omega Seme, Shamte Ally, Idrisa Rashid, Kiggi Makassy,
 
Washambuliaji; Kenneth Asamoah, Pius Kisambale, Davies Mwape, Jeryson Tegete
 
Aidha Benjamin Berko aliyekuwa majeruhi kwa mda mrefu, tayari amepona na amaenza mazoezi mepesi ikiwa ni pamoja na kufanya mazoezi ya ufukweni.
 
Salum Telela anaendelea na matibabu ya kifundo cha mguu
 
Hamis Kiiza anaendelea na matibabu ya mbavu zilizomsababisha asicheze mechi ya Cairo 
Last Updated ( Thursday, 08 March 2012 09:08 )  

 

   
  • FACEBOOK PAGE

  • TWITTER FEEDS

yanga1935: Uongozi wa mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya Vodacom klabu ya Young Africans leo umekata mzizi wa fitina kwa kiungo... http://t.co/oZUqXpuAyz
yanga1935: Droo ya makundi kwa ajli ya mashindano ya Vilabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati al-maarufu kama (KAGAME CUP)... http://t.co/r2esjJLwtJ
yanga1935: Katibu Mkuu wa klabu ya Young Africans Lawrence Lawrence Mwalusako leo amemtambulisha rasmi kwa waandishi wa... http://t.co/fkfqNHiwz1
yanga1935: Green and yellow colours were dominant from the early hours of Saturday and it went on to be the dominant colours... http://t.co/sshr7bjgeQ
yanga1935: I posted 5 photos on Facebook in the album "CHAMP24NS" http://t.co/jw1L47m1kO
yanga1935: Sherehe za kukabidhiwa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2012/2013 kwa Mabingwa wapya Young Africans... http://t.co/S8GiejZjr7
yanga1935: Mpira umemalizika, Young Africans 2 - 0 Simba SC Kavumbagu ddk 4 Kiiza dkk 63
yanga1935: Dakika ya 89, Mpira umesimama kidogo, baada ya Nassoro Chollo kumsukuma Kavumbagu na wakati mwamuzi anamuulia kadondoka chini mwenyewe.
yanga1935: Dakika ya 85, anaingia Juma Abdul kuchukua nafasi ya Mbuyu Twite
yanga1935: Dakika ya 75, Young Africans 2 - 0 Simba SC Anaingia Nizar Khalfani kuchukua nafasi ya Hamis Kiiza
yanga1935: Dakika ya 75, Young Africans 1 - 0 Simba SC Anaingia Nizar Khalfani kuchukua nafasi ya Hamis Kiiza
mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday3073
mod_vvisit_counterYesterday6215
mod_vvisit_counterThis week27390
mod_vvisit_counterLast week19559
mod_vvisit_counterThis month69734
mod_vvisit_counterLast month60138
mod_vvisit_counterAll days558764

We have: 26 guests, 3 bots online
Your IP: 54.234.126.92
 , 
Today: May 25, 2013